
Kiukweli Mangwea alikufa kifo cha masikitiko, msanii huyo aliyewai kutamba na wimbo wa Geto langu pamoja na mikasi iliyotengenezwa na mwaandaaji wa ala za muziki nchini Tanzania P Funk Majani.
Mangwea alikutwa amekufa katika chumba walichokuwa wamelala na msanii wa mwenzake M 2 The P, Mangwea alikutwa amelowa damu nyingi, ambazo zilikuwa zikitoka kwa wingi kupitia mdomoni,puani na masikioni.
Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo wameiambia Hot92tanzania.blogspot.com kwamba kitendo cha msanii huyo kuvuja damu nyingi ndiyo iliyosababisha kifo chake na kwamba hata jopo la Madaktari waliompokea walishangazwa na damu hizo kabla ya uchunguzi kufanyika.
Kwa upande mwingine, mkurugenzi wa Utafiti na Matukio wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba
"Tumeamua kwa mikono miwili
kushiriki katika msiba huu wa ndugu yetu Mangwea,” alisema kwa ufupi. Ngwea amepangwa kuletwa
Tanzania kesho Jumamosi na kuagwa Jumapili, kabla ya kupelekwa mkoani Morogoro
kwa ajili ya mazishi yake.
Barua inayoonyesha walioanza kuchangia msiba wa Ngwea.
Na Kambi Mbwana, Dar es
Salaam
KAMPUNI
ya Clouds FM,
imejitolea kuusafirisha mwili wa marehemu Albert Mangwea kwa ajili ya
kuutoa
Afrika Kusini hadi Tanzania kwa ajili ya kuzikwa, ukiwa ni utaratibu
unaoonyesha kuwa wadau wote wameamua kushirikiana katika suala hili.
No comments:
Post a Comment