Monday, July 29, 2013

Hili NDILO JIWE LA AJABU NCHINI TANZANIA NA HAIRUHUSIWI KULIPANDA WALA KULISOGELEA!!

Haya ndio maajabu ya JIWE LA MBUJI wilayani Mbinga, Ruvuma.

Maana ya neno "MBUJI" ni "Kitu Kikubwa"
  1. Baada ya utafiti wa mkoa wa Ruvuma, ndilo jiwe pekee kubwa mkoani humo.
  2. Lina vyanzo vingi vya maji
  3. Huwezi kulipanda mpaka uombe kibali kutoka kijijini hapo. Na ukithubutu kulipanda bila ya ruhusa, unaweza ukafa. Na tayari kuna Mzungu mmoja alikuja kwaajili ya utali, akapanda hilo jiwe bila idhini na akakutwa amepoteza maisha.
  4. Ni vigumu kulizunguka. Unaweza ukazunguka na usifike mwisho, hata kama uliweka alama, hutoikuta.
  5. Jiwe la Mbuji hutumika kwaajili ya matambiko kwa baadhi ya koo za eneo hilo.
  6. Kuna watu maalumu wanaotoa maelekezo kwa yeyote anaetaka kulisogelea au kulipanda.
  7. Ni kivutio kikubwa kwa wageni wanaotembelea vijiji vya Litembo, Maguu, Hagati nk. huko Mbinga, Ruvuma.
  8. Linaheshimika sana kwa wakazi wanaolizunguka jiwe hilo.
  9. Sehemu kubwa ya watu wanaoishi karibu na jiwe hilo, hawajawahi kulizunguka wala kulipanda kutokana na hofu.
  10. Jina la jiwe hilo ndio tarafa ya Mbuji wilayani Mbinga.
 ********************************************************************************

These are the wonders of Mbuji stone, Mbinga District, Ruvuma, Tanzania.

The meaning of the word "Mbuji" is "Something Big"

  1. After research on Ruvuma region, it is  the region's biggest stone. 
  2. Has many sources of water.
  3. You  cannot climb till you request permission from the village. And if you dare climb without permission, you can die. And already there is a European who came in favor of tourism, climbed the rock without permission and he was found dead.
  4. You can  hardly circle the rock. Also, you can go around and do not bar the end, even if you leave a mark. 
  5. Mbuji stone is used for rituals in favor of some of the families of the area.
  6. There are special people who give instructions to anyone who wants to climb the stone. 
  7. It is a major attraction for visitors who visits Litembo, feet, Hagati villages etc. in Mbinga District, Ruvuma, Tanzania.
  8. The stone is very respected by the people around the area.
  9. A large proportion of people living near that stone, out of fear, they have neither climbed nor circled the stone.
  10. Name of the stone is the division of  Mbuji, Mbinga District.

HATIMAYE MBOWE AWASILISHA USHAHIDI POLISI KUHUSU MLIPUAJI WA BOMU ARUSHA

HATIMAYE Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, jana amewasilisha kwa maandishi ushahidi wake makao makuu ya Jeshi la Polisi mjini Dar es Salaam.

Maelezo ya Mbowe ambayo jana yaliwasilishwa, yamekuwa siri nzito, kwani yanatokana na msimamo wa CHADEMA kudai wana ushahidi na tukio la mauaji ya mlipuko wa bomu lililotokea Juni 15, mwaka huu mkoani Arusha.
 
Wakili wa Mbowe, Peter Kibatala alilithibitishia MTANZANIA mjini Dar es Salaam jana, kuwa aliwasilisha saa 5 asubuhi ambapo alipokelewa na Mkuu wa Idara ya Operesheni za Upelelezi Tanzania (CID), Kamishna Advocate Nyombi.

Baada ya kuwasilisha maelezo hayo, Wakili Kibatala alikataa katakata kuzungumzia kilichomo ndani ya maandishi hayo, kwa madai kuwa ni siri yao na polisi.

“Nathibitisha bila shaka, nimewasilisha majibu kwa niaba ya Mbowe leo (jana), makao makuu ya polisi kama tulivyokubaliana, lakini yaliyoandikwa humo ni siri…siwezi kuzijadili tusubiri kutoka kwao,” alisema Kibatala.

Hatua ya kuwasilisha majibu hayo kimaandishi, ilifikiwa Jumatano wiki hii katika mahojiano baina ya Polisi na Mbowe.

Siku hiyo, Mbowe aligoma kuwasilisha ushahidi wake polisi kama alivyotakiwa kwenye barua aliyoandikiwa na jeshi hilo Julai 17, mwaka huu, kwa kile alichosema hadi Rais Jakaya Kikwete atakapounda tume ya kijaji kuchunguza tukio hilo.

Katika barua hiyo, Mbowe alitakiwa kufika bila kukosa akiwa na ushahidi wa mauaji ya mlipuko wa bomu hilo.

Hata hivyo, Mbowe aliripoti kuitikia wito wa barua hiyo, lakini aliendelea kushikilia msimamo wake wa kutowasilisha ushahidi huo kwa polisi.

Jeshi la Polisi, limekuwa katika mvutano na Mbowe likimtaka kuwasilisha ushahidi kuhusu mlipuko wa bomu hilo, katika Uwanja wa Soweto wakati wa mkutano wa kuhitimisha kampeni za uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata nne na kuua watu wanne na kujeruhi wengine 70, katika uwanja huo ushahidi ambao alidai anao.

Endapo Mbowe atakutwa na hatia ya kutokuwa na ushahidi huo, atakumbwa na adhabu ya miaka mitatu jela au faini ya Sh 500,000.

Hii ni kwa mujibu wa Jeshi la Polisi katika barua yake kwa Mbowe, ikunukuu kifungu cha sheria ya kifungu cha 10(2) na (2A) cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai nchini, sura ya 20, kama ilivyorekebishwa mwaka 2002

Tuesday, July 2, 2013

Kifuta Jasho


Mpango wa AGOA ulioiingizia Tanzania Sh92.8trilioni

Wafanyabiashara Tanzania watumia asilimia 8

Ukuzaji fursa za kiuchumi Afrika, (African Growth and Opportunity Act), AGOA, ni mpango mahsusi ulioanzishwa kwa ajili ya kuziwezesha nchi za Afrika kuuza bidhaa zao nchini Marekani.

Mpango huo upo kwa mujibu wa sheria baada ya kupitishwa Mei 18, 2000 na kwamba mpango huo unasaidia nchi za Afrika ikiwamo Tanzania kuuza bidhaa zao, kukuza mitaji pamoja na kupanua masoko kiuchumi.

Aliyekuwa Rais wa Marekani, George W. Bush alitia saini Mkataba wa Biashara kati ya Mataifa ya Afrika na Amerika, kupitia AGOA mwaka 2004.

Tanzania ambayo ni mmoja wa wanachama wa AGOA, ni miongoni mwa nchi zinazofaidika na mpango huo kwa kuuza bidhaa mbalimbali Marekani na kuingiza Sh92.8 trilioni hadi mwaka 2011, ikiwa ni zaidi ya asilimia 36.

Mwaka 2010, mauzo ya bidhaa za Tanzania nchini Marekani yaliingiza Dola 15 milioni (Sh24 bilioni) ikiwa ni juu ya asilimia 73.1 tangu mwaka 2000.

Makubaliano ya biashara

 Mbali na mpango wa AGOA, Marekani ilisaini mkataba uitwao; Trade and Investment Framework Agreements (TIFA) na nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka 2008, na Soko la Pamoja kwa Nchi za Kusini na Mashariki (Comesa) mwaka 2001. Tanzania ni mwanachama wa jumuiya zote hizo.

Marekani imekuwa ikijaribu mpango wake wa biashara na Afrika Mashariki na hata mwakilishi wake, katika masuala ya biashara Balozi, Ron Kirk aliwahi kuitembelea Tanzania kwa mara ya kwanza mwaka huo, 2011 lengo ni kuimarisha uhusiano wa biashara kati ya Tanzania na Marekani.

Tanzania ni kati ya mataifa 136 yanayofanya biashara na Marekani na tangu kipindi hicho, jumla ya biashara za kuuza na kununua zinafikia Dola 316 milioni. Tanzania ni nchi ya 121 inayosafirisha kwa wingi bidhaa zake kwenda Marekani.

Kwa mwaka 2011, Marekani iliuza bidhaa zake Tanzania zenye thamani ya Dola 258 milioni, sawa na asilimia 57.7, ikiwa ni zaidi ya Dola 94 milioni tangu mwaka 2010, na zaidi ya asilimia 474.7 tangu  mwaka 2000.

Nchi hiyo pia imenunua kutoka Tanzania mashine mbalimbali za Dola 61 milioni, ngano (Dola 53 milioni), bidhaa za nguo (Dola25 milioni), mpira (Dola 15 milioni), na mashine za umeme za Dola 13 milioni.
Kwa mazao ya kilimo, Marekani ilinunua; kahawa, viungo, chai zilizoliingizia taifa Dola 29 milioni, madini (Dola 9 milioni, Knit Apparel Dola 5 milioni), mbogamboga ziliingiza Dola 5 milioni, matunda, korosho Dola 2 milioni na kahawa iliyoingiza Dola 28 milioni.

Kimsingi, Marekani na Tanzania ni washirika wakubwa katika biashara hasa katika Ukanda wa nchi zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara. Nchi hiyo iko katika harakati za kuwekeza kupitia mpango wake wa Millennium Challenge Account, Feed the Future na Partnership for Growth (PFG).

PFG, ni mpango wa kwanza wa Rais Barack Obama kwa ajili ya kukuza uchumi wa nchi zinazoendelea, demokrasia na utawala bora.

Nafasi za biashara

 Pamoja na kuwapo kwa nafasi za kuuza bidhaa mbalimbali nchini Marekani kupitia AGOA, wafanyabiashara wanatumia asilimia nane pungufu ya nafasi zinazotolewa na Marekani.

Kutokana na hali hiyo, Serikali inawataka wafanyabiashara kutumia nafasi hiyo kwa ajili ya kukuza kipato chao na cha taifa kwa kufanya biashara na taifa hilo lililostawi kiuchumi.

Akizungumza kwenye Mkutano wa mwaka wa TCCIA, Juni mwaka huu, Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk  Abdallah Kigoda, anasema pamoja na kuwepo wigo mpana wa biashara kama; AGOA, Jumuiya ya Afrika Mashariki, (EAC), Umoja wa Ulaya (EU), Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afika (Sadc), Tanzania inashiriki katika Jumuiya hizi katika nafasi ndogo.

 “Ni wakati wa wafanyabiashara kuzalisha mali kwa wingi na bora, kisha kuuza nje ikiwamo katika jumuiya mbalimbali zenye wigo mpana wa biashara,” anasema Dk Kigoda.

Dk Kigoda anasema, TCCIA lazima itoe elimu kwa wanachama wake, hasa kuhusu umuhimu wa uzalishaji na usindikaji mali ulio bora na kuuza nje ili kuongeza pato kwa mkulima kwa mazao bora.

Uwekezaji wa Marekani Tanzania

Aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC, Raymond Mbilinyi anasema  uwekezaji wa taasisi za nje nchini, umekua kwa asilimia 10 na ulitarajiwa kuingiza Dola13 bilioni hadi kufikia mwishoni mwa 2012.

Hata hivyo, China inaonekana kuteka sehemu kubwa ya uwekezaji Afrika Mashariki ikiwamo Tanzania ikilinganishwa na Marekani. Mpaka sasa, China imewekeza Dola1.4 bilioni ikiwa ni zaidi ya Marekani ambayo imewekeza Dola950 milioni Tanzania.

Ujio wa Rais Barack Obama  leo unaweza kuongeza wigo wa nchi yake kuwekeza Tanzania hasa kupitia mpango wa Millennium Challenge Corporation, MCC.

Akithibitisha hayo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe anasema uwekezaji utaongezeka kupitia mpango wa MCC, ambao utafadhili masuala ya elimu, afya na miradi ya barabara.

MCC, ni mpango ulioasisiwa na Baraza la Congress la Marekani mwaka 2004 kwa ajili ya kusaidia nchi zinazoendelea, na mwaka 2011 uliisaidia Tanzania Dola 698 milioni kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo.

“Tanzania imekuwa ikipata misaada ya MCC kwa elimu, miundombinu na afya...tutafanya mazungumzo kuhusu masuala ya kiuchumi, nishati Afrika na maendeleo ya uchumi na jinsi ya njia mbalimbali za uwekezaji.”

Mpango mwingine uliopo katika kukuza uchumi ni kupitia Millennium Challenge Account, MCA, ambao kazi yake ni kuendeleza sekta ya usafiri, umeme na maji.

Obama, Bush ana kwa ana Tanzania

Rais wa Marekani, Barack Obama na mtangulizi wake, George W. Bush, leo wanakutana ana kwa ana kwenye ardhi ya Tanzania watakapoweka mashada kwenye Ubalozi wa zamani wa Marekani uliolipuliwa mwaka 1998.

Rais Obama ameweka rekodi ya kuwa mtu wa kwanza mweusi kuchaguliwa kuongoza Marekani, akipokea wadhifa huo kutoka kwa Rais Bush, ambaye aliiongoza taifa hilo kuanzia mwaka 2000-2008.

Kitendo cha vigogo hao kukutana nchini ni cha kihistoria na kinadhihirisha jinsi Marekani ilivyoipa kipaumbele Tanzania kwa masuala ya diplomasia.
Viongozi hao wawili, wapo Tanzania wakati Rais Obama akimalizia ziara yake ya Afrika na Bush atakuwa na mkewe, Laura, watahudhuria mkutano wa wake za marais wa Afrika unaodhaminiwa na Taasisi ya Bush Foundation.

Pia, Michelle Obama, atahudhuria mkutano huo kabla ya kuondoka kurejea Marekani.
Balozi mbili za Marekani za Dar es Salaam na Nairobi, Kenya zilishambuliwa kwa wakati mmoja Agosti 7, 1998. Obama ataweka shada kama sehemu ya kumbukumbu ya tukio hilo na Bush ataungana naye katika shughuli hiyo.

Hata hivyo, viongozi hao hawatahutubia wakati wa shughuli hiyo.
Rais Obama ametoa pongezi kwa sera za Bush Afrika hasa kwa kuongoza mapambano dhidi ya ugonjwa hatari wa Ukimwi.

Hata hivyo, utawala wa Rais Obama umejikita zaidi katika mapambano dhidi ya ugaidi.
Kuna kamandi ya Jeshi ya Africom, ambayo ina kazi kubwa ya kukabiliana na ugaidi barani humu.Operesheni kubwa za Africom zipo nchi za Afrika Kaskazini, Somalia na Afrika ya Kati ambako wanamsaka kiongozi wa Kundi la Waasi la Lord Resistance, Joseph Kony.

Monday, July 1, 2013

Obama awasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius K. Nyerere Dar Es Salaam majira ya saa nane na dakika arobaini mchana

Rais wa Marekani Barack Obama amewasili nchini Tanzania leo Jumatatu, ikiwa ni kituo chake cha mwisho cha ziara yake barani Afrika akitokea nchini Afrika Kusini.

Akiwa nchini Tanzania rais Obama atafanya mazungumzo na rais wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete  na waandishi wa habari na kisha kutembelea kituo cha umeme cha Ubungo , baada ya kuahidi kutoa dola za Marekani bilioni saba kusaidia mradi wa umeme Barabi Afrika.

Mpango huo wa serikali ya Marekani utazinduliwa kwanza katika nchi za Ethiopia, Ghana, Kenya, Liberia, Nigeria na Tanzania ambazo wananchi wake wanakumbwa na matatizo ya upatikanaji wa umeme.

Aidha Obama ameeleza kuwa Afrika itakuwa na mustakabali mzuri kwa kuwa na viongozi wanaopambana kuhakikisha raia wao wanakuwa na maisha bora.
Katika ziara yake nchini Afrika Kusini , Obama hakusita kusifu jitihada za kiongozi wa zamani na baba wa taifa hilo Nelson Mandela ambaye ameeleza kuwa jitihada zake za ukombozi kwa raia wa taifa hilo zilimsukuma kuingia katika siasa na hatimaye kuwa rais wa kwanza mweusi nchini Marekani

Friday, June 28, 2013

BET Awards 13 Live on Sunday June 30th...... Hosted by Chris Tucker

The Black Entertainment Television (BET) Awards 2013 is underway and to be hosted by Actor and Comedian CHRIS TUCKER

Featuring the following nominees...
  1. Best Female R&B/POP artist
    • Beyonce Knowles
    • Tamar Braxton
    • Alicia Keys
    • Rihanna
    • Elle Varner
     2.  Best Male R&B/POP Artist
    • Chris Brown
    • Bruno Mars
    • Miguel
    • Justin Timberlake
    • Usher
     3.  Best Group
    • Macklemore & Ryan Lewis
    • Mary Mary
    • Mindless Behaviour
    • Slaughter-House
    • The Throne (Jay z & Kanye West)
     4.  Best Collaboration
    • 2Chainz f/ Drake - No Lie
    • A$AP Rocky f/ Drake, 2Chainz & Kendrick Lamar - Problems
    • French Montana f/ Rick Ross, Drake & Lil Wayne - Pop That
    • Kendrick Lamar f/ Drake - Poetic Justice
    • Justine Timberlake f/ Jay Z - Suit & Tie
    • Kanye West f/ Big Sean, Pusha T & 2Chainz - Mercy
     5.   Best Male Hip Hop Artist
    • 2Chainz
    • A$AP Rocky
    • Drake
    • Future
    • Kendrick Lamar
     6.   Best Female Hip Hop Artist
    • Azealia Banks
    • Eve
    • Nicki Minaj
    • Rasheeda
    • Rye Rye
     7.    Video Of The Year
    • 2Chainz f/ Drake - No Lie
    • A$AP Rocky f/ Drake, 2Chainz & Kendrick Lamar - Problems
    • Drake - Started From The Bottom
    • Drake f/ Lil Wayne - HYFR
    • Kendrick Lamar f/ Drake - Poetic Justice
    • Macklemore & Ryan Lewis f/ Wanz - Thrift Shop
    • Miguel - Adorn
    • Rihanna - Diamonds
    • Justine Timberlake f/ Jay Z - Suit & Tie
    • Kanye West f/ Big Sean, Pusha T & 2Chainz - Mercy
      8.   Video Director Of The Year
    • A$AP Rocky & Sam Lecca
    • Benny Boom
    • Director X
    • Dre Films
    • Hype Williams
       9.   Best New Artist
    • Azealia Banks
    • Joey Bad A$$
    • Kendrick Lamar
    • Trinidad Jame$
    • The Weeknd
      10.   Best Gospel Artist
    • Deitrick Haddon
    • Lecrae
    • Tamela Mann
    • Mary Mary
    • Marvin Sapp
      11.   Best Actress
    • Angela Bassett
    • Halle Berry
    • Taraj P. Henson
    • Gabrielle Union
    • Kerry Washington
      12.   Best Actor
    • Don Cheadle
    • Common
    • Jamie Foxx
    • Samuel L. Jackson
    • Denzel Washington
      13.   Subway Sportswoman Of The Year
    • Gabrielle Douglas
    • Brittney Grinner
    • Candace Parker
    • Serena Williams
    • Venus Williams
      14.   Subway Sportsman Of the year
    • Ray Lewis
    • Kevin Durant
    • LeBron James
    • Victor Cruz
    • Robert Griffin III
      15.   Coca-Cola Viewers Choice Awards
    • A$AP Rocky f/ Drake, 2Chainz & Kendrick Lamar - Problems
    • Drake - Started From The Bottom
    • Kendrick Lamar - Swimming Pools (Drank)
    • Miguel - Adorn
    • Rihanna - Diamonds
    • Justine Timberlake f/ Jay Z - Suit & Tie
      16.   Centric Awards
    • Tamar Braxton - Love & War
    • Fantansia - Lose To Win
    • Miguel - Adorn
    • Nas - Daughters
    • Charlie Wilson - My Love Is All I Got
      17.   Best International Act: Africa
    • 2Face Idibia
    • Toya Delazy
    • Donald
    • Ice Prince
    • R2Bees
    • Radio & Weasel
      18.   Best International Act: UK
    • Marsha Ambrosius
    • Estelle
    • Labrinth
    • Emeli Sande
    • Rita Ora
    • Wiley
The People who'll perform on the night.......
  • Janell Monae
  • T.I
  • Robin Thicke
  • Justin Timberlake
  • Snoop Dogg
  • Mariah Kelly
  • Nicki Minaj
  • Ciara
  • Miguel
  • Kendrick Lamar
  • Chris Brown
  • R Kelly
  • Stevie wonder
  • Erykah Badu
  • India.Arie
  • Charlie Wilson
 
DON'T MISS THE FUN.........!!!!! LIVE ON BET SUNDAY 28TH OF JUNE 7PM EAT

Mwanamke Mbeya Matatani Kwa Kuua Mume

MWANAMKE mmoja mkazi wa kijiji cha Iganduka wilayani Mbozi Mkoani Mbeya makrina Simbowe (42) anashikiliwa na jeshi la polisi Mkoani hapa kwa kosa la kumuua mumewe aitwaye Rodrick Mwaipasi (55)baada ya mwanamke huyo kuuza karanga debe mbili bila idhini ya mume wake.
 
Tukio la kifo cha mwanaume huyo linatokana na marehemu kuhoji kwa mke wake juu ya kuuza karanga debe mbili bila idhini yake na hivyo mwanamke huyo kumsukuma mume wake ambaye aliangukia kisogo na kufariki papo hapo.
 
Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake Kamanda wa polisi Mkoani Mbeya Bw.Diwani 
Athuman alisema tukio hilo limetokea juni 24 mwaka huu majira ya saa 2.00 usiku katika kijiji cha Iganduka wilayani hapa
 
Baada ya marehemu kusukumwa alidondoka na kupelekwa katika hospitali mbozi mission ambapo hata hivyo alikuwa ameshafariki kutokana na kuangukia kisogo.
Aidha Diwani alisema chanzo cha mzozo huo ugomvi wa kifamilia uliotokea kati yao kisha marehemu kusukumwa na mke wake na kufariki dunia.
 
Hata hivyo Kamanda Athuman alisema kuwa mtuhumiwa amekamatwa na taratibu zinafanywa ili afikishwe mahakamani ,na kutoa wito kwa jamii kutatua matatizo/migogoro yao kwa njia ya mazungumzo badala ya kujichukulia sheria mkononi kwa kutumia hasira na nguvu.

Mandela ni simanzi

NI simanzi kila kona ya dunia! Baba wa Taifa la Afrika Kusini na kipenzi cha Waafrika kwa jumla, Nelson Rolihlahla Madiba Mandela (94), ameibua simanzi baada ya familia yake kukutana kwenye eneo la makaburi ya ukoo kwa ajili ya kuandaa mazishi ya rais huyo wa kwanza mweusi wa nchi hiyo. 



 Hayo yanakuja kufuatia afya ya mzee huyo kuwa tete akisumbuliwa na maradhi ya mapafu ambapo leo anatimiza siku 20 tangu alipokimbizwa katika Hospitali ya Mediclinic Heart iliyopo jijini Pretoria, Afrika Kusini ‘Sauzi’.
 

Historia ya matatizo ya mapafu ya Mzee Madiba ilianza alipokuwa kwenye Gereza la Kisiwa cha Robben karibu na Cape Town kwa miaka 27 ambapo aliachiwa huru mwaka 1990 na akaendelea kutumikia nchi kama rais wa kwanza wa Afrika Kusini huru kuanzia mwaka 1994 hadi 1999.

Habari zilieleza kuwa kabla ya kwenda katika makaburi hayo ya ukoo yaliyopo katika Kijiji cha Qunu jimboni Eastern Cape kwenye makazi ya Mzee Madiba, familia nzima ilikutana kwa ajili ya kikao cha siri lakini haikujulikana mara moja walichokijadili.
 
WAANDISHI WAPIGANA VIKUMBO
Hata hivyo, waandishi wa Sauzi na vyombo vya kimataifa kama vile BBC, CNN, Sky News na wengine wengi ambao tayari wamejazana kijijini hapo, walizuiwa mita chache getini kwani hawakutakiwa kujua kilichokuwa kinajadiliwa na familia.

Kuhusu safari ya makaburini ilielezwa kuwa ni mila za watu wa Kabila la Xhosa ambapo wanaukoo hulazimika kwenda kwenye makaburi kufanya tambiko wanapohisi kuna mtu wa ukoo huo ataaga dunia muda mfupi mbele.

“Mzee Madiba alishaonesha mahali atakapozikwa, ni kwenye makaburi ya ukoo wa Madiba walipozikwa ndugu zake wengine ndiyo maana walikwenda kupafanyia ‘mambo’,” uliandika mtandao mmoja wa Sauzi.
Kwa upande wake mkewe, Graca Machel alilazimika kuahirisha safari yake ya kikazi ili kuwa karibu naye huku mkewe wa zamani ambaye walitalikiana mwaka 1996, Winnie Madikizela Mandela akiwa miongoni mwa wanafamilia waliojumuika kushirikiana katika maandalizi hayo.
 
HALI YA KIJIJI CHA QUNU
Habari zinasema kuwa Kijiji cha Qunu kimetawaliwa na vilio na simanzi kubwa zinazoongozwa na ukoo wa Madiba kama ilivyo dunia nzima ambapo macho na masikio ya wengi yameelekezwa nchini humo.
 
 MAANDALIZI MAKUBWA
Tayari kumekuwa na maandalizi makubwa ya kumpumzisha kiongozi huyo huku wageni wakiendelea kumiminika Sauzi kwa kuamini si wa kupona tena.
 
BARABARA KIWANGO CHA LAMI
Habari zilizidi kueleza kuwa tayari kuna matengenezo ya barabara kwa kiwango cha lami kutoka Eastern Cape hadi kijijini hapo huku greda likionekana kwenye uwanja mkubwa uliopo kwenye makazi ya Mzee Madiba.
 
UWANJA WA NDEGE
Pia kuna matengenezo makubwa ya Uwanja wa Eastern Cape ambao umefikia kwenye kiwango cha kutua ndege kubwa aina ya Boeing 737 kwa ajili ya wageni watakaokwenda kijijini Qunu.
 
UJIO WA OBAMA
Kwa mujibu wa sosi wetu Sauzi, ujio wa Rais wa Marekani, Barack Obama umeingia shubiri nchini humo kwa vile habari ya mjini ni Mzee Madiba hivyo shamrashamra za kumpokea rais huyo hazina nguvu  ‘automatiki’.
Kuhusu hilo, imeelezwa kuwa Obama hataruhusiwa kwenda kumuona Madiba jambo lililoibua maswali kuwa iweje rais mkubwa kama huyo asiende kumjulia hali kiongozi huyo mkubwa duniani.
 
HISTORIA
Mzee Madiba alizaliwa Julai 18, 1918 katika kijiji kidogo cha Mvezo kilichoko katika Wilaya ya Umtata Jimbo la Eastern Cape nchini humo.
Jina lake lingine la katikati la Rolihlahla linamaanisha ‘kuvuta tawi la mti’ au ‘mleta matatizo’ huku Madiba likiwa jina lake la utotoni.
 
HARAKATI
Baada ya ushindi katika uchaguzi wa mwaka 1948 wa Chama cha Kiafrikana cha National Party (NP), ambacho kiliunga mkono sera za utengano wa  kibaguzi, Mzee Madiba alianza kushiriki harakati za kisiasa.
Mzee Madiba aliongoza kampeni maarufu ya uasi ya Chama cha ANC mwaka 1952 na 1955 katika harakati za kupigania ukombozi wa mtu mweusi.

Katika kipindi hicho, Madiba na mwanasheria mwenzake na rafiki yake mkubwa, Oliver Tambo, waliendesha Kampuni ya Sheria ya Mandela na Tambo, wakitoa ushauri wa kisheria bure au kwa gharama ndogo kwa wazalendo weusi waliokosa uwakilishi wa kisheria.
 
UBAGUZI
Mwaka 1961, Madiba alikuwa kiongozi wa Kundi la Kijeshi la ANC, Umkhonto we Sizwe ambalo tafsiri yake ni ‘Mkuki wa Taifa’ ambalo pia lilipewa ufupisho wa MK na alishiriki kuliunda na mwenzake mwingine.
Aliendesha kampeni za hujuma dhidi ya jeshi na maeneo ya serikali na kufanya mipango ya kuwezesha vita ya msituni iwapo hujuma zitashindwa kumaliza ubaguzi wa rangi.
 
KUKAMATWA
Agosti 5, mwaka 1962, Madiba alikamatwa baada ya kuishi akizikimbia mamlaka husika kwa miezi 17 na akafungwa katika ngome ya Johannesburg Fort huko Sauzi.

Kukamatwa kwake kunadaiwa kufanikishwa na makachero wa Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA), waliozigusia mamlaka za usalama Afrika Kusini aliko Mandela.

Siku tatu baadaye, mashitaka ya kuendesha mgomo na kuondoka nchini isivyo halali mwaka 1961 yakasomwa mahakamani, Oktoba 25, 1962 alifungwa jela miaka mitano.
 
GEREZANI
Baada ya kutiwa hatiani kwa kesi ya uhaini, Juni 12, 1964, Mahakama ilitoa adhabu ya kifungo cha maisha jela kwa Madiba na wenzake.

Madiba alifungwa jela katika Gereza la Kisiwa cha Robben ambako alikaa kwa kipindi cha miaka 27.
Wakati akiwa jela, umaarufu wake uliongezeka na kujulikana kama kiongozi muhimu kabisa wa wazalendo weusi Afrika Kusini.

KUACHIWA
Februari 2, 1990, kaburu Rais Frederik Willem de Klerk alibatilisha amri inayoipiga marufuku ANC na taasisi nyingine zilizopinga ubaguzi wa rangi na akatangaza kwamba Madiba ataachiwa kutoka jela muda si mrefu.
Mandela aliachiwa kutoka gerezani Februari 11, 1990, tukio hilo lilitangazwa duniani kote.
 
AFRIKA KUSINI MPYA
Baada ya shujaa Madiba kuachiwa, majadiliano ya kumaliza ubaguzi wa rangi nchini humo  yakafuata.
Madiba alirudi katika uongozi wa Chama cha African National Congress (ANC) kati ya mwaka 1990 na 1994.

Uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi wa Afrika Kusini isiyo ya kibaguzi ulifanyika Aprili 27, 1994 ambapo ANC ilishinda kwa asilimia 62 na Madiba kama kiongozi wa ANC aliapishwa Mei 10, 1994 kuwa rais wa kwanza mweusi.
 
NDOA
Mandela alioa mara tatu na kujaliwa watoto sita, wajukuu 20 na idadi kubwa ya vitukuu.
 
NDOA YA KWANZA
Ndoa ya kwanza ya Madiba alifunga na Evelyn Ntoko Mase ambaye alizaa naye watoto wawili.
Wawili hao waliachana mwaka 1957, walitalikiana baada ya harakati zake za ukombozi huku mkewe akiwa Shahidi wa Yehova, dini ambayo ilihitaji kutosimama upande wowote kisiasa.
 
NDOA YA PILI
Ndoa ya pili ya Madiba ilikuwa na Winnie Mandela ambaye alionana naye Johannesburg akiwa mfanyakazi wa kwanza mweusi wa jiji.

Madiba na Winnie walijaliwa mabinti wawili, Zenani (Zeni), aliyezaliwa mwaka 1958 na Zindziswa (Zindzi) Mandela-Hlongwane, aliyezaliwa 1960.

Wakati mume wake akitumikia kifungo cha maisha, baba wa Winnie alikuwa Waziri wa Kilimo katika Jimbo la Transkei. Ndoa yao ilivunjika Aprili 1992 na talaka kufikiwa Machi 1996, ikichangiwa na mtengano mrefu wa kisiasa.
 
NDOA YA TATU
Madiba alioa tena katika kumbukumbu yake ya siku ya kuzaliwa ya kutimiza miaka 80 ya mwaka 1998.
Wakati huu alimuoa Graca Simbine Machel, mjane wa aliyekuwa Rais wa Msumbiji, marehemu Samora Machel na mshirika wa ANC ambaye alikufa katika ajali ya ndege mwaka 1986.
 
MARADHI
Madiba alikuwa rais mkubwa kabisa kuchaguliwa Afrika Kusini wakati alipoingia madarakani akiwa na umri wa miaka 75 mwaka 1994, alidhamiria kutowania muhula wa pili na alistaafu mwaka 1999, akirithiwa na Thabo Mbeki.

Julai 2001, Madiba aligundulika kuwa na saratani ya kibofu ambapo alitibiwa kwa mionzi kwa kipindi cha wiki saba.

Mwaka 2003, kifo cha Madiba kilitangazwa kimakosa na Shirika la Habari la Marekani (CNN).
Mwaka 2007, kundi la mrengo wa kulia lilisambaza barua pepe bandia na ujumbe wa simu za mikononi kuwa mamlaka zimeficha kifo cha Madiba na kwamba weupe nchini humo watauawa baada ya mazishi yake.

Wakati hayo yakitokea, Madiba alikuwa mapumzikoni nyumbani kwa mkewe Msumbiji.
Juni 2004, akiwa na umri wa miaka 85, Madiba alitangaza kuwa anajiuzulu katika shughuli za kijamii.
Siku ya kutimiza miaka 90 ya kuzaliwa ya Madiba ilisherehekewa nchini kote Julai 18, mwaka 2008, huku sherehe kubwa ikifanyika kijijini kwake Qunu.

Pamoja na kutojionesha sana wakati wa michuano ya Kombe la Dunia iliyofanyika nchini humo mwaka 2010, Madiba alionekana wakati wa sherehe za ufunguzi.

Januari 2011, alilazwa katika hospitali binafsi ya Millpark, jijini Johannesburg kwa kile kilichoelezwa kipindi hicho na taasisi yake kuwa uchunguzi wa kawaida na kuibua minong’ono mizito katika vyombo vya habari kuhusu kuzidi kuzorota kwa afya yake kabla ya hivi karibuni hali kuwa mbaya akisumbuliwa na mapafu.

Usafi wa Jiji hadi aje Rais Obama?

Kuelekea ujio wa Rais Barack Obama nchini wiki ijayo, Jiji la Dar es Salaam ambalo ndilo litakuwa mwenyeji wa mgeni huyo na ujumbe wake hivi sasa limo katika hekaheka kubwa za kuandaa mazingira stahiki kwa ugeni huo. Dar es Salaam ni moja ya majiji machafu sana duniani, hivyo kila juhudi zinafanywa na mamlaka husika kuliweka jiji hilo katika hali ya usafi kabla ya ugeni huo haujawasili.

Sasa sehemu nyingi za barabara zinatengenezwa usiku na mchana kwa kujengwa upya au kuzibwa mashimo, ambayo baadhi yake yalikuwa makubwa mithili ya mahandaki. Katika baadhi ya barabara, mchanga na udongo uliokuwa umezimeza kutokana na kutotunzwa kwa muda mrefu sasa vimeondolewa.

Taka zilizokuwa zimezagaa kila kona sasa zinazolewa kwa kutumia magari ya Jiji na ya wamiliki binafsi. Katika sehemu muhimu za Jiji, madawa ya kuua mbu na wadudu yamenyunyizwa, huku baadhi ya wamiliki wa majengo katika sehemu atakazopita Rais Obama wakilazimika kupaka rangi majengo hayo. Harufu mbaya iliyokuwa imeligubika Jiji kutokana na uchafu sasa imepungua kwa kiasi kikubwa.

Ghafla vijana kutoka vijiweni wamepewa ajira ya muda kufyeka nyasi, kuzibua na kusafisha barabara na mitaro iliyojaa majitaka. Kumbe wanakaa vijiweni sio kwa kutaka, bali kwa kukosa ajira. Polisi nao wameendesha kamatakamata ya vijana wengi inaodai ni vibaka, wavuta bangi na vitendo vingine vya kihalifu, huku lengo kubwa likiwa ni kusafisha mitaa kabla ya ujio wa Rais Obama. Wakati huohuo, Machinga wameondolewa katika sehemu atakazopita mgeni huyo na ujumbe wake na vibanda vyao vimefyekwa na tingatinga za Jiji, huku wananchi waishio mikoani wakitahadharishwa kutokuja Dar es Salaam wakati Rais Obama atakapokuwa jijini.

Jiji la Dar es Salaam zinazoendelea hivi sasa jijini kuelekea ujio wa ugeni wa Rais huyo wa Marekani. Tumefanya hivyo kwa sababu mbili kubwa. Kwanza ni kuonyesha kwamba Jiji la Dar es Salaam na Serikali Kuu vinao uwezo mkubwa wa kulifanya jiji hilo kuwa safi wakati wote. Pili ni kuonyesha jinsi tunavyojidhalilisha kama taifa kwa kuishi katika mazingira machafu, lakini tunachukua hatua za zimamoto na kukimbizana kufanya usafi tunapoona wageni wanatembelea nchi yetu.

Ni aibu iliyoje kwa Watanzania kuishi katika mazingira machafu tukisubiri wageni waje ndio tufanye usafi. Ni dharau na matusi ya viongozi wetu kwa wananchi, kwamba watu muhimu na ambao wanastahili kuwekwa katika mazingira mazuri ni wageni. Wananchi wanasakamwa walipe kodi na wanafanya hivyo. Pamoja na kulipa kodi hizo, mamlaka husika hazioni umuhimu wa kuwatengenezea wananchi mazingira mazuri kwa kuzoa taka, kutengeneza barabara, kufyeka nyasi, kunyunyizia dawa katika mazalio ya mbu na kadhalika.

Usafi wa mazingira na wa kila mwananchi ni muhimu mno katika ustawi na maendeleo ya binadamu. Wakati kila mwananchi analo jukumu la kutunza usafi kwa nafsi yake na mazingira yaliyomzunguka, mamlaka husika zinapaswa kuwawezesha wananchi kufanya hivyo. Inawezekanaje halmashauri za miji na wilaya, kwa mfano, zishindwe kuweka magari ya kuzoa taka kutoka barabarani na mitaani? Zipo wapi dampo za kumwaga maelfu ya tani za taka zinazozalishwa katika makazi ya watu mijini kila siku?

Madege 8 ya Obama yatua Dar

Habari zilizopatikana kutoka kwa wafanyakazi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere,zinasema kuwa helikopta sita zinaunganishwa katika sehemu ya karakana ya Kikosi cha Anga cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Dar es Salaam. Makachero wa Marekani wameendelea na matayarisho ya mwisho ya ziara ya Rais Barack Obama, ambapo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere walikuwa na kazi ya kuunganisha helikopta za doria.

Makachero hao walikuwa wakiunganisha helikopta sita zilizosafirishwa vipande vipande kutoka Marekani, ambapo meli mbili za kivita na ndege moja pia zimewasili.
Rais Obama tayari yuko katika ardhi ya Afrika, ambapo leo anatarajiwa kwenda Afrika Kusini baada ya kumaliza ziara yake ya kwanza Senegal na anatarajiwa kuwasili nchini Jumatatu.

Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa jana na Mwananchi unaonyesha Marekani imeleta helikopta hizo kwa ajili ya ulinzi wa Rais Obama, zikiwemo meli zilizobeba helikopta nyingine mbili na ndege.
Habari zilizopatikana kutoka kwa wafanyakazi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere,zinasema kuwa helikopta sita zinaunganishwa katika sehemu ya karakana ya Kikosi cha Anga cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Mpashaji mmoja aliliambia gazeti hili kuwa helikopta hizo zililetwa kama vipande vipande vilivyosafirishwa kama mzigo kwenye meli za kivita zilizotia nanga jijini Dar es Salaam.
“Nilikaribia kwenye eneo la karakana na nikashangaa kuona jinsi jamaa walivyokuwa ‘bize’ wakiunganisha vyuma mbalimbali na kutengeneza helikopta hizo,” aliongeza mpashaji wetu, ambaye alibahatika kusogelea eneo hilo licha ya kuwepo kwa ulinzi mkali.

Inaaminika kuwa helikopta hizo zitakuwa zinasaidia kusafirisha watu na mizigo kutoka kwenye meli za kivita ambazo zimeegeshwa kwenye Kikosi cha Maji cha JWTZ.
Pia helikopta mbili zinaaminika ziko katika meli ambazo zimeegeshwa huko Kigamboni.
Meli za kivita na ndege ya kijeshi

Katika hatua nyingine, meli mbili za kivita ambazo zimetengenezwa kwa teknolojia ya hali ya juu zimeegeshwa Kigamboni.
“Jamaa wana meli kali kwa kweli, mimi nimekuwa askari wa Kikosi cha Maji kwa muda mrefu na kufanya mazoezi na mataifa kadhaa, lakini sijaona meli kama zile.

“Wamarekani wanatisha sana. Meli zao zina zana muhimu za kivita. Pia wanafuatilia kila kitu kinachoweza kuhatarisha usalama wao. Hawaamini mtu kabisa wala kudharau chochote,” aliongeza mtoa habari mmoja.
Ndege ya kijeshi
Taarifa zaidi zinaeleza kuwa kuna ndege ya Jeshi la Marekani lakini imeegeshwa kwenye karakana ya Kikosi cha Anga cha JWTZ.

Ndege hiyo inadaiwa iko nchini tangu mwanzoni mwa wiki hii, ingawa kuna taarifa kuwa zipo ndege nyingine ambazo zimekuwa zikitua na kuruka.
“Ndege nyingi za Wamarekani zinatua nchini kwa kipindi cha wiki mbili sasa, zaidi zinaleta watu, ambao nahisi ni wale wanaohusika na usalama na mizigo.
“Kimsingi kuna mambo mengi yanaendelea hapa uwanja wa ndege. Ila msisahau pia kuna ujio wa marais kutoka sehemu mbalimbali duniani kwa ajili ya mkutano wa Smart Partnership ndiyo maana kuna mengi yanaendelea hapa,” kiliongeza chanzo chetu.

Matapeli waibuka

Kuna habari pia, kuna kundi la watu limeibuka jijini Dar es Salaam ambalo linataka kutapeli wakazi wa jiji kwa kutumia mgongo wa ujio wa Rais wa Marekani, Barack Obama.
Kamishna wa Polisi wa Kanda Maalumu, Suleiman Kova aliliambia gazeti hili kuwa wamepelekewa kesi tatu za majaribio ya watu kupora wengine kwa kutumia mgongo wa Obama.

Ziara ya Rais Obama imesababisha kuongezeka kwa mahitaji ya usafiri na malazi, hali iliyosababisha kuibuka kwa matapeli wanaowalenga watu wenye magari yenye hadhi kwa wageni wa nje.
Pia hali hiyo imechangiwa zaidi kutokana na ugeni wa viongozi wapatao 11 kutoka mataifa mbalimbali duniani, wanaohudhuria mkutano wa Smart Partnership unaoanza leo jijini Dar es Salaam.
Kova alisema kundi hilo limekuwa likiwasiliana na watu wanaomiliki magari ya kifahari ili wakodishe magari yao.
 
“Matapeli huwa wanajifanya kuwa wanawakilisha Ubalozi wa Marekani na kujifanya wanataka magari ili kubeba watu watakaofuatana na Rais Obama.
Kwa mujibu wa Kova matapeli hao walilenga kutumia ziara ya Rais Obama kufanikisha wizi wa magari, hasa yale ya kifahari.

Kituo cha Mabasi cha Mwenge chasafishwa
Katika hatua nyingine, Manispaa ya Kinondoni ilivunja vibanda vya biashara kwenye Kituo cha Mabasi cha Mwenge.
Operesheni hiyo iliendeshwa kwa ushirikiano wa maofisa wa Manispaa, Askari wa Jiji, Kikosi cha Polisi cha Kutuliza Fujo (FFU).

Watu walioshuhudia tukio hilo wanaeleza kuwa wafanyabiashara ndogondogo walikuwa wakikimbia ovyo huku wakiwa wamebeba bidhaa zao.
Kituo hicho cha Mwenge huwa kina wachuuzi wengi na wengine hufikia hatua ya kuweka vitu chini.
Mkutano wa Smart Partnership

Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue amesema macho na masikio ya dunia nzima kuanzia leo yanahamia jijini Dar es Salaam kutokana na ugeni mkubwa wa marais tisa na ujumbe wa watu 800, kutoka nchi mbalimbali duniani wanaoanza leo mkutano wa majadiliano ya Smart Partnership.
Mkutano wa Smart Partnership unahusu uwekezaji katika sayansi na teknolojia kwa lengo la kujiletea maendeleo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Sefue alisema mkutano huo utafunguliwa na Rais Jakaya Kikwete katika Ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Nyerere jijini Dar es Salaam.
“Nchi yetu imepata heshima kubwa, macho na masikio dunia nzima sasa yanaitazama Tanzania, kila mgeni atakuwa balozi wetu wa kuitangaza nchini yetu huko ughaibuni,” alisema Sefue.

Marais watakaohudhuria katika majadiliano hayo na nchi zao kwenye mabano ni Yoweri Museveni (Uganda), Uhuru Kenyatta (Kenya), Boni Yayi (Benin), Ali Omar Bongo (Gabon), Ikililou Dhoinine (Comoro), Ernest Koroma (Sierra Leone) na Blaise Compaore (Burkina Faso).
Viongozi wengine ni Mfalme Mswati II (Swaziland) na Mahinda Rajapaska (Sri Lanka), ambao wametua nchini tayari ya mkutano huo.
Imeandikwa na Beatrice Moses, Patricia Kimelemeta na Ramadhani Kaminyonge

OUT kumtunuku Obama PhD

Kwa mujibu wa Profesa Mbwete, Rais Obama anakuwa mtu wa tano kutunukiwa tuzo hiyo baada ya kutanguliwa na Mwalimu Julias Nyerere, Rais wa kwanza mweusi wa Afrika ya Kusini, Nelson Mandela, Rais wa awamu ya tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Benjamin Mkapa.

Dar es Salaam. Chuo Kikuu Huria Tanzania (OUT),kimepanga kumtunuku Rais wa Marekani, Barack Obama Shahada ya Heshima ya Uzamivu kwa kutambua mchango wake kwa jamii husasani kwenye maendeleo ya kukuza uchumi.

Akizungumza na waandishi wa habari jana,Makamu Mkuu wa chuo hicho,Profesa Tolly Mbwete alisema tuzo hiyo imethibitishwa na Baraza Kuu la Chuo hicho baadaye kupitishwa na Mkuu wa OUT, Dk Asha Rose Migiro.

“Tumeangalia vigezo vyote muhimu ambavyo mtu anastahili kupewa tuzo kama hii na tukaridhika kuwa Rais huyo anastahili kutunukiwa,” alisema Profesa Mbwete.

Kwa mujibu wa Profesa Mbwete, Rais Obama anakuwa mtu wa tano kutunukiwa tuzo hiyo baada ya kutanguliwa na Mwalimu Julias Nyerere, Rais wa kwanza mweusi wa Afrika ya Kusini, Nelson Mandela, Rais wa awamu ya tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Benjamin Mkapa.

Alisema hadi sasa OUT imetoa shahada saba za heshima, ambapo kati ya hizo mbili walitunukiwa mwanataaluma kutoka Marekani, Dk Jane Goodall na Mhadhiri wa Mawasiliano kutoka nchini Uingereza,David Mellor.

Thursday, June 13, 2013

Nyundo ya mwisho Kagame Cup

WAKATI serikali ikibariki rasmi kuwa timu za Simba, Yanga na Falcon ya Zanzibar hazitashiriki michuano inayoandaliwa na Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (Cecafa), Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limesema haliwezi kupingana na uamuzi huo.

Jana bungeni mjini Dodoma, Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla, alitoa kauli rasmi ya serikali, wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Sumve, Richard Ndassa.
Ndassa katika swali lake alitaka kujua msimamo wa serikali kama timu za Tanzania zitashiriki michuano hiyo ambayo imo shakani kutokana na baadhi ya mataifa kuanza kujitoa kutokana na hali duni ya usalama nchini Sudan.

Akijibu swali hilo, Makalla alisema ni kweli kumekuwa na taarifa za kutokuwa na usalama nchini Sudan na kwamba Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe, alishalitolea ufafanuzi.

“Sisi ndani ya serikali tuna taarifa za kutosha kuwa Sudan Kusini hakuna usalama na nchi nyingine zimeendelea kujitoa, hivyo msimamo wetu kama serikali hatuwezi kupeleka timu sehemu isiyo na usalama,” alisema Makalla.

Juni mosi mwaka huu, Waziri Membe wakati akihitimisha hotuba ya bajeti ya wizara yake alisema kwamba, anashangaa kuona Sudan ikipewa uenyeji wa michuano hiyo licha ya kuwa na usalama mdogo.

Alisema kwa mujibu wa sheria za kimataifa, kwenye nchi zenye machafuko ili michuano kama hiyo iweze kufanyika ni lazima sehemu husika wanakofikia wachezaji na maofisa wengine kuwe na magari maalumu ya kuzuia risasi (bullet proof) ya kuwabeba kutoka uwanja wa ndege hadi sehemu wanakokwenda.
Waziri Membe alihoji busara iliyotumiwa na Cecafa kuteua nchi hiyo kuwa mwenyeji wa michuano hiyo inayotarajiwa kuanza Juni 18.

Akizungumzia hali hiyo jana, Katibu Mkuu wa TFF Angetile Osiah, alisema serikali ndiyo yenye mamlaka ya mwisho juu ya suala hilo na kama imeona hali hairuhusu kwa Simba na Yanga kwenda huko, hawana budi kuheshimu uamuzi huo.

“Haya mashindano yapo chini ya Cecafa, hivyo hatuwezi kuyazungumzia zaidi, lakini kama wasimamizi wa soka nchini hatuna budi kufuata maelekezo ya serikali, kwani ndiyo ina uamuzi wa mwisho,” alisema.
Nao viongozi wa Simba na Yanga, wakizungumzia hatua ya serikali kuzizuia kushiriki michuano hiyo kwa wakati tofauti kila upande ulidai kutokuwa na taarifa rasmi na kuahidi kutoa tamko pindi watakapozipata.

Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako, ambao timu yao ni mabingwa watetezi, alisema hawawezi kulizungumzia hilo hadi watakapopata taarifa rasmi ndipo uongozi utakutana na kutoa tamko rasmi.
Mwalusako aliongeza kwamba, timu yake imekuwa katika maandalizi si kwa ajili tu ya ushiriki wa michuano hiyo, kwani kuna Ligi Kuu, Klabu Bingwa ya Afrika na hata mechi kadhaa za kirafiki.

Naye Kaimu Makamu Mwenyekiti wa Simba, Joseph Itang’are ‘Kinesi’, alisema wakipata rasmi taarifa ya serikali uongozi utakutana na kuamua nini cha kufanya.

Nyundo ya mwisho Kagame Cup

WAKATI serikali ikibariki rasmi kuwa timu za Simba, Yanga na Falcon ya Zanzibar hazitashiriki michuano inayoandaliwa na Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (Cecafa), Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limesema haliwezi kupingana na uamuzi huo.

Jana bungeni mjini Dodoma, Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla, alitoa kauli rasmi ya serikali, wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Sumve, Richard Ndassa.
Ndassa katika swali lake alitaka kujua msimamo wa serikali kama timu za Tanzania zitashiriki michuano hiyo ambayo imo shakani kutokana na baadhi ya mataifa kuanza kujitoa kutokana na hali duni ya usalama nchini Sudan.

Akijibu swali hilo, Makalla alisema ni kweli kumekuwa na taarifa za kutokuwa na usalama nchini Sudan na kwamba Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe, alishalitolea ufafanuzi.

“Sisi ndani ya serikali tuna taarifa za kutosha kuwa Sudan Kusini hakuna usalama na nchi nyingine zimeendelea kujitoa, hivyo msimamo wetu kama serikali hatuwezi kupeleka timu sehemu isiyo na usalama,” alisema Makalla.

Juni mosi mwaka huu, Waziri Membe wakati akihitimisha hotuba ya bajeti ya wizara yake alisema kwamba, anashangaa kuona Sudan ikipewa uenyeji wa michuano hiyo licha ya kuwa na usalama mdogo.

Alisema kwa mujibu wa sheria za kimataifa, kwenye nchi zenye machafuko ili michuano kama hiyo iweze kufanyika ni lazima sehemu husika wanakofikia wachezaji na maofisa wengine kuwe na magari maalumu ya kuzuia risasi (bullet proof) ya kuwabeba kutoka uwanja wa ndege hadi sehemu wanakokwenda.
Waziri Membe alihoji busara iliyotumiwa na Cecafa kuteua nchi hiyo kuwa mwenyeji wa michuano hiyo inayotarajiwa kuanza Juni 18.

Akizungumzia hali hiyo jana, Katibu Mkuu wa TFF Angetile Osiah, alisema serikali ndiyo yenye mamlaka ya mwisho juu ya suala hilo na kama imeona hali hairuhusu kwa Simba na Yanga kwenda huko, hawana budi kuheshimu uamuzi huo.

“Haya mashindano yapo chini ya Cecafa, hivyo hatuwezi kuyazungumzia zaidi, lakini kama wasimamizi wa soka nchini hatuna budi kufuata maelekezo ya serikali, kwani ndiyo ina uamuzi wa mwisho,” alisema.
Nao viongozi wa Simba na Yanga, wakizungumzia hatua ya serikali kuzizuia kushiriki michuano hiyo kwa wakati tofauti kila upande ulidai kutokuwa na taarifa rasmi na kuahidi kutoa tamko pindi watakapozipata.

Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako, ambao timu yao ni mabingwa watetezi, alisema hawawezi kulizungumzia hilo hadi watakapopata taarifa rasmi ndipo uongozi utakutana na kutoa tamko rasmi.
Mwalusako aliongeza kwamba, timu yake imekuwa katika maandalizi si kwa ajili tu ya ushiriki wa michuano hiyo, kwani kuna Ligi Kuu, Klabu Bingwa ya Afrika na hata mechi kadhaa za kirafiki.

Naye Kaimu Makamu Mwenyekiti wa Simba, Joseph Itang’are ‘Kinesi’, alisema wakipata rasmi taarifa ya serikali uongozi utakutana na kuamua nini cha kufanya.

Hapatoshi Taifa, Diamond Vs Prezzo

MKALI wa muziki wa kizazi kipya hapa nchini, Naseeb Abdul ‘Diamond’ na mkali wa hip hop kutoka Kenya, Jackson Makini ‘Prezzo’, wanatarajia kupanda jukwaa moja kwenye Tamasha la Usiku wa Matumaini litakalofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Julai 7 mwaka huu.

Kwa mujibu wa Mratibu wa tamasha hilo, Abdallah Mrisho ‘Abby Cool’, mpambano huo unatarajiwa kutegua kitendawili cha ‘Nani Mkali’ kati ya wasanii hao kwenye Ukanda wa Afrika Mashariki na kudai kuwa ana imani itakuwa burudani murua kwa wakazi wa jiji na mikoa ya jirani.

Alisema Diamond ambaye ana tuzo ya Msanii Bora wa Kiume ya KTM, ataoneshana ubavu na mkali Prezzo, ambaye ndiye anayeongoza kwa kupendwa nchini Kenya, hivyo unatarajiwa kuwa mpambano mkali kwa kuwa utakuwa ni kati ya Bongo Fleva na hip hop.

Aliongeza kuwa mpambano huo ambao unahusisha Kenya na Tanzania, kwa upande wa ngumi kutakuwa na Patrick Amonte kutoka Kenya na Thomas Mashali wa Tanzania huku Shadrack Machanje akizichapa na Francis Miyeyusho.

“Ukiachana na ngumi, pia bendi za Msondo Ngoma, Jahazi Modern Taarab na Sikinde zitakuwapo kuhakikisha wanakidhi haja za mashabiki wote watakaojitokeza siku hiyo, huku TMK Halisi na Wanaume Family watawafundisha mashabiki wao staili mpya za uchezaji wao, hivyo hii si ya kukosa,” alisema.

Alivitaja viingilio kuwa ni sh 20,000 kwa VIP, viti vya bluu sh 10,000 na mzunguko sh 5,000. Tiketi zitaanza kuuzwa mapema na vituo husika vitatajwa baadaye.

AFTER EARTH STREAMING WATCH FULL MOVIE PCTV ONLINE FREE MEGAVIDEO

Mzozo wa ving’amuzi watua bungeni

SERIKALI imetakiwa kuruhusu matumizi ya teknolojia ya analojia sambamba na dijitali hadi hapo nchi itakapokuwa tayari kuendana na mabadiliko hayo ya kiteknolojia.

Mapendekezo hayo yalitolewa bungeni jana na Mbunge wa Kasulu Mjini, Moses Machali wakati akiwasilisha maelezo binafsi kuhusu matumizi sambamba kati ya teknolojia ya dijitali na analojia.
Machali alisema kuwa utaratibu wa kuzima mitambo ya analojia kwa mikoa mingine usitishwe hadi hapo vituo vya luninga vitakapokuwa na uwezo wa kurusha matangazo yao moja kwa moja kwa kutumia teknolojia hiyo ya dijitali.

“Serikali izingatie hali ya kipato cha matumizi bila kujali matakwa ya kiteknolojia au ya kibiashara. Utu wa Mtanzania ni vyema ukatazamwa kwa jicho la utaifa zaidi,” alisema.

Machali alisema kuwa serikali ina jukumu la kuhakikisha wananchi wote waliokuwa wanapata matangazo ya luninga kwa njia ya analojia wanapata sambamba kwa njia ya dijitali. Alisema kuwa ili kupata matangazo hayo ya dijitali, mwananchi anahitaji kisimbuzi (king’amuzi), kwamba visimbuzi viko vya aina mbili; DVB-T na DVB-T2.

“Kisimbuzi cha DVB-T2 kinaweza kupokea matangazo kutoka kwenye mitambo ya DVB-T2 na DVB-T. Kisimbuzi cha DVB-T kinaweza kupokea matangazo kutoka kwenye mitambo ya DVB-T peke yake,” alisema. Machali alisema kuwa tatizo la kuhamia katika teknolojia ya dijitali ni kubwa kwa wamiliki wa vituo vya luninga na kwa wananchi wa kawaida. Kwamba maamuzi ya kuhamia kwenye teknolojia hiyo yamefanywa kwa haraka sana.

Alisema kuwa bila kufanya utafiti, kwa kulinganisha tu idadi ya mitambo ya analojia iliyokuwepo na ya dijitali iliyopo, ukweli huo unajidhihirisha kwenye mikoa mfano Dodoma kulikuwa na mitambo sita ya analojia; ITV, EATV, TBC, Star tv, Channel 10 na Agape.

Kwamba sasa hivi kuna mitambo miwili tu ya dijitali ya Star Media na Agape Associates wakati Mwanza kulikuwa na mitambo sita ya analojia; ITV, EATV, TBC, Star tv, Channel 10 na Agape TV lakini sasa ipo miwili ya Star Media na Agape Associates.

CCM watumia udiwani kufanya kampeni za urais

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM na mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Abdallah Bulembo, wiki hii aligeuza kampeni za uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata za Kaloleni, Elerai, Kimandolu na Themi, jijini Arusha kuwa za urais 2015 kwa kuwashambulia Dk. Willibrod Slaa wa CHADEMA na Profesa Ibrahim Lipumba wa CUF.

Bulembo aliyekuwa akihutubia mkutano wa kampeni eneo la Stadium Bar kumnadi mgombea wa CCM Kata ya Kaloleni, alitumia muda mrefu kupiga propaganda za uchaguzi mkuu ujao badala ya kumnadi mgombea hali iliyowafanya wananchi wachache waliohudhuria mkutano huo kupaza sauti za kumtaka kutangaza sera badala ya kuzungumzia watu.

Kama vile hakusoma mazingira na nyuso za wasikilizaji wake ambao walionekana dhihiri kuchukizwa na hotuba yake, Bulembo aliwaomba Watanzania kutompigia kura za urais Dk. Slaa akidai atawaasi kama alivyoacha upadri na “kuoa mtawa, Rose Kamili.”

Kamili ni mzazi mwenzake Dk. Slaa, lakini hajawahi kuwa mtawa.

Kuhusu Profesa Lipumba, kada huyo wa CCM alidai asichaguliwe kwa sababu ni mzoefu wa kushindwa baada ya kuanza harakati za kuwania kiti cha urais tangu uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vingi mwaka 1995 hadi sasa.

“Sifa ya maprofesa ni kufanya tafiti na kuandika vitabu vya kitaaluma. Sasa huyo Profesa Lipumba atakuja kuandika kitabu cha uzoefu wa kushindwa urais? Hafai huyu na kamwe Watanzania msimchague 2015. Mimi ni mjumbe wa CC na ninaahidi CCM tutawaletea mgombea safi,” alisema Bulembo na kuzua minong’ono miongoni mwa wasikilizaji.

Baadhi ya washiriki wa mkutano huo walisema kitendo cha Bulembo kuacha kumnadi mgombea na kugeukia kumshambulia Dk. Slaa ni dalili kuwa CCM inamhofia katibu huyo mkuu wa CHADEMA katika uchaguzi mkuu ujao 2015.

Dk. Slaa hajatangaza kugombea urais, lakini mvuto wake na upinzani mkubwa aliouonyesha dhidi ya Rais Jakaya Kikwete katika uchaguzi uliopita bado unaitia kiwewe CCM, hasa iwapo uchaguzi huo utafanyika kwa kutumia katiba mpya itakayounda tume huru ya uchaguzi tofauti na ya sasa inayodaiwa kukipendelea chama hicho tawala.

Katika uchaguzi uliopita, Dk. Slaa alipata zaidi ya kura milioni mbili nyuma ya Rais Kikwete ingawa kulikuwapo tuhuma za uchakachuaji na ushiriki wa vyombo vya dola kuibeba CCM na wagombea wake.

Kenyan MPs 'agree to lower salaries'

Kenya's MPs have agreed to drop their annual salary by $45,000 ($28,700) to $75,000 following a public outcry, a government-appointed body has said.
The MPs would receive a car allowance of around $58,000, for agreeing to the cut, the Salaries and Remuneration Commission (SRC) said.
On Tuesday, protesters in the capital, Nairobi, denounced MPs as "MPigs".
MPs voted for a $120,000 annual salary in May, in defiance of the wishes of the SRC and President Uhuru Kenyatta.
'Trade-off' They argued they deserved the amount because they worked hard and gave financial help to their constituents.
But their decision sparked national outrage as the MPs are among the highest paid in the world and the average income in Kenya is around $1,800 a year.
MPs agreed to the pay cut of nearly 40% in "fruitful" talks held with them, the SRC said.
The 416 MPs would receive a one-off car grant of around $58,000, as it was a "more viable option" than giving each of them a chauffeur-driven car, the SRC added, AFP news agency reports.
The MPs would also receive hefty pension benefits, it reports.
MPs in the previous parliament awarded themselves a $107,000 retirement bonus in one of the last sessions before the election.
The package also provided them with an armed guard, a diplomatic passport and access to airport VIP lounges.
Kenya held presidential and parliamentary elections in March.
The SRC and the president can only recommend how much MPs should earn - they cannot take a decision.

Nelson Mandela 'responding better' to treatment for lung infection after five days in hospital

Mandela spent a fifth straight day in hospital where he was visited by one of his daughters and three grandchildren.


Nelson Mandela is responding better to treatment after several days in hospital, says South African president Jacob Zuma. South Africa’s parliament burst into applause as they heard the news about the 94-year-old anti-apartheid hero and Nobel prize winner. Mandela spent a fifth straight day in a Pretoria hospital today where he was visited by one of his daughters and three grandchildren.. Grandson, Mandla Mandela, said the family has been deeply touched by the outpouring of prayers and messages of goodwill from around the world. He added the family is satisfied with the care Mandela is receiving.

Today marked the 49th anniversary of the sentencing of Mandela to life in prison in 1964. President Zuma said “our thoughts” are with Mandela and his family “on this crucial historical anniversary.”
“We are very happy with the progress that he is now making following a difficult last few days,” he added.
“We appreciate the messages of support from all over the world.
“We fully understand and appreciate the global interest in this world icon. We are so proud to call him our own.
“We urge South Africans and the international community to continue to keep President Mandela and the medical team in their thoughts and prayers."

Mandela, the leader of South Africa’s anti-apartheid movement, spent 27 years in prison during white racist rule. He is being treated for a recurring lung infection. His fourth stay in hospital since December. Mandela - who is 95 next month - contracted tuberculosis during his imprisonment on windswept Robben Island off Cape Town where he was forced to break rocks by hand in a stone quarry. He was freed in 1990. US President Barack Obama and Michelle Obama have wished Mandela a “speedy recovery”. His admission to a hospital in Pretoria, the capital, is Mandela’s fourth stay in hospital for treatment since December.

Security at the hospital remains tight. Even the movement of medical staff is restricted. One medic said: “It’s crazy. From yesterday no one can come in or out without being stopped and searched. There are certain floors to which access, even for medical staff, has been limited.” Stairwells are under guard and lifts are being monitored.

Monday, June 3, 2013

Higuain: I have decided to leave Real Madrid

Real Madrid striker Gonzalo Higuain has confirmed that he wishes to leave the club when the transfer window reopens.
 
The Argentina international was named stand-in captain as Jose Mourinho’s men rounded off the 2012-13 campaign with a 4-2 home victory over Osasuna on Saturday.
 
He opened the scoring in the 35th minute with a well-taken finish, and played the entirety of the match as Real took the win courtesy of a flurry of late goals.
 
Mourinho had already announced that he would depart the Santiago Bernabeu after the final Liga game of the season, but it now appears that he will be joined by Higuain – who has revealed he has had offers from other clubs.
 
“I feel that my time here is over, I want a change,” he said.
“These seven years have been intense, hard and bright. It was a considered decision. It wasn’t easy, but I think I want to go to another club, new challenges.
 
“I hope Madrid do what is best for me. This is a decision that has been taken.”
Higuain has previously been linked with Italian champions Juventus, and has now admitted such a move would appeal to him.
 
He added: “Juventus and other teams are interested in me. Juventus is an historical club and many great players have played there.
“I want to go where I can prove myself really. I have several offers and want a change of scenery.
“I was never given anything here, I always had to fight for the death. I came for €12 million but I think I will sell for more.”
 
Should he leave Real, Higuain will finish his spell with the Madrid club having scored 122 goals in 266 appearances.

Arsenal Have Agreed Pre-Contract Deal to Sign Barcelona Striker David Villa According to Spanish Sources

Emirates Stadium side closing in on Spanish international.


Arsenal have reportedly secured a pre-contract agreement with Barcelona striker David Villa according to a report from talkSPORT.

The 31 year old Spanish international has long been linked with a move to the Emirates Stadium with Arsene Wenger plotting a move for the Nou Camp bit-part player in January, now it appears that as part of those talks a deal has been put in place that could be triggered this summer.

Spanish journalist Axel Torres says he’s been informed by a senior source that Barcelona striker David Villa wants to move to England, with the Spain international reportedly showing the club’s board an pre-contract agreement to sign for Arsenal if the Catalan giants allow him to move.

Wenger may well see Villa as an ideal supporting striker as he continues to show faith in Olivier Giroud and Lukas Podolski as two players he believes have a great deal to offer his North London attack.

David Villa has started just 17 La Liga matches, netting ten goals in the process.

With the arrival of Neymar likely to further limit his involvement the former Valencia man may well feel that he needs regular first team football at this stage of his career, not least as there is a World Cup on the horizon.

Rihanna - Rihanna offers condolences to Bruno Mars

Rihanna has sent Bruno Mars her condolences after his mother died in a hospital in Hawaii from a brain aneurysm on Saturday (01.06.13).
 

Rihanna has sent her condolences to Bruno Mars after the death of his mother.
The 'Diamonds' singer sent the star - real name Peter Hernandez - support on twitter after his mother passed away on Saturday (01.06.13) She tweeted: ''Sending my love and condolences to Bruno Mars at this difficult time! I'm sincerely praying for you bro! #1Love (sic).''

Bruno's mother, Bernadette Hernandez, was admitted to hospital in Honolulu, Hawaii in a critical condition on Friday (31.05.13), but died the next day of a brain aneurysm.

Rihanna can sympathise with Bruno as last year she lost her beloved grandmother, Clara 'Dolly' Braithwaite, and had to cancel shows to fly back to her native Barbados to be with her family and grieve.
A number of other celebrities have since written to Bruno, 27, to offer their support during this difficult time.
Actress Jennifer Love Hewitt - who lost her mother Patricia to cancer last year - wrote: ''My heart is breaking for Bruno Mars and his family tonight. I know all too well, too recent and too deep what they are feeling. Nothing in the world like a mother. And nothing can prepare you for the pain of losing one. Sending my condolences.''

Singer Boy George tweeted: ''Bruno Mars Thoughts and prayers to you fella. I'm sorry for your loss. Our mothers are goddesses.''
'Glee' star Amber Riley wrote: ''No worse feeling than losing a loved one. My condolences. Prayers for Bruno Mars.''

Tamko rasmi la "push mobile" na "bongo records kuhusu mauzo ya nyimbo ya marehemu Ngwair


Kim Kardashian Baby Gender: What Is It?!?

The water may still be intact, but the news broke on last night's Keeping Up with the Kardashians Season 8 premiere:

Are Kim and Kanye West having a boy or a girl?!?

And the answer was revealed early:
"I don't see any pee-pees," Dr Crane said at his client's visit: "I'm thinking it's a GIRL."
"Oh my gosh! What's the percentage?" replied Kim.

Upon being told it was 99, Kim gushed: "I am so excited to be having a girl. Who doesn't want a girl?!?" Kardashian then added that boyfriend West (not actually at the ultrasound) has always wanted a girl, as she pondered whether her daughter would be musical and concluded:
"I just can't wait to see what she's going to talk like and look like. I am so excited about the joy she is going to bring into our lives."

So, let the prediction game begin: What will Kim Kardashian name her little girl?

Sunday, June 2, 2013

Tanzania: President Kikwete Says No to Kigali Demand for Apology

Dodoma — PRESIDENT Jakaya Kikwete will not apologise for the advice he made to Rwandan Government to enter into talks with rebels to end 16 years of war because the country has failed to settle the matter through combat.
The Minister for Foreign Affairs and International Cooperation, Mr Bernard Membe told the National Assembly that the remarks made by President Kikwete during the 21st African Union Summit on May 26th, this year in Addis Ababa, Ethiopia were in good faith.
"Rwanda have issued a statement opposing the advice by President Kikwete that this was the right time to hold peace talks with the country rebels most of whom are in DRC forests and whom the government has unsuccessfully fought for nearly 17 years," he said.
The Ministers said Tanzania saw the presence of such rebels in the DRC forests as a setback in the region's peace process. Mr Membe who was speaking shortly before the House approved his ministry's 2013/14 budget estimates added:
"President Kikwete will not apologise because his statement was based on facts. We ask Rwanda to take this advice. Our President cannot apologise for the truth." He reminded Rwanda to remember the fact that peace was to be made with enemies and that negotiations should be made with enemies and not friends.
"We (Tanzania) and Rwanda are friends, we have nothing to negotiate, but they should know that principally we ought to make peace with enemies and negotiate with our enemies and not friends," he said.
He added that there have been talks with terrorist organisations where they existed including in South Africa where ANC was regarded as terrorist group.
"We say that President Kagame should admit that the time is now and this is not a new phenomenon because in all the areas where liberation movements are, talks have been made.
What we are saying is that President Kagame and Rwandan government should know that it is time for talks with opposition," he insisted. Rwanda's Minister of Foreign Affairs, Louise Mushikiwabo was on Monday quoted in an interview with Radio France Internationale (RFI), saying that Rwanda would not consider negotiating with Democratic Forces for the Liberation of Rwanda (FDRL).
Mushikiwabo's remarks came days after President Kikwete made peace talk remarks asking Rwanda and Uganda to consider talks with the FDLR rebels. The Rwandan Chairperson of Parliament's Foreign Affairs committee, MP Gideon Kayinamura also stated that the idea of suggesting negotiations with the FDLR militias is a big insult to Rwandans.
Rwandans living in the US have also petitioned the US President Baraka Obama give a blind ear to such remarks and continue with its support to Rwanda and the region in bringing the FDLR criminals to justice.
The US government has already reinstated a five million US dollar bounty on the FDLR rebel leaders, like Sylvestre Mudacumura and labelled the group as a terrorist movement in the region.
Meanwhile, Mr Membe told the National Assembly that the government would consider taking to DRC eight journalists to cover the country's peacekeeping forces in the Eastern side of the country.
"Our forces in DRC are doing a wonderful job and they have been received with jubilation and we hope they will keep the spirit alive by demonstrating our values and hospitality," he said.
Mr Membe, however, noted that there is propaganda aimed at mudslinging the country forces and thus plans were underway to send eight reporters under army guidance to report the country's forces activities.
"We will soon send eight reporters to DRC where they will document activities by our forces which are already there for peace restoration in the Eastern part of the country," he said. A total of 1,283 soldiers are due to be sent to Congo from Tanzania to form the UN Force Intervention Brigade (FIB) made up of 3069 soldiers in total.

Kizunguzungu kuhusu muafaka wa mwili wa marehemu Albert Mangwea. . . . . . ..

Leo asubuhi, taarifa kutoka Johannesburg S.A, inasema kuwa, mwili wa marehemu Albert Mangwea a.k.a Ngwair, utaendelea kubaki katika hospitali ya St. Helen iliyopo Johannesburg S.A hivyo atasafirishwa kesho kuja Tanzania.

Kauli hiyo iliyotoka leo majira ya saa tatu asubuhi, imeleta maswali mengi miongoni mwa watanzania. Wengi wanajiuliza ni kwanini mwili wake uhairishwe kusafirishwa mara ya pili, iwapo haijatolewa sababu yoyote ya msingi.

Safari ya kwanza ya kuuleta mwili wa marehemu ngwair ilikuwa ni jumamosi lakini wakahairisha kutokana na maombi ya kuuga mwili huo kwa watanzania waishio Afrika kusini, na kusema unaweza kusafirishwa leo na kuingia saa nane mchana kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere Aiport jijini Dar Es Salaam. Napo hiyo safari imehairishwa na kupanga kesho ndio mwili huo unaletwa Tanzania.

Sababu iliyotoka ni kwamba wanahofia usalama wa safari yenyewe kitu ambacho si cha msingi. Na kuleta maswali mengi kuto kwa wakazi wa jiji la Dar Es Salaam.

"Mimi nahisi kuwa mwili wa mshikaji wetu (ngwair) umebaki tena labda kwaajili ya uchunguzi wa madaktari, koz inaweza ikawa jamaa aliwekewa sumu, hivyo basi wamembakiza huko ili wafanye uchunguzi huo" alisema mkazi mmoja wa mitaa ya sinza kumekucha (jina limehifadhiwa).

Je! hii ni kwa sababu gani??



Saturday, June 1, 2013

Rehema Chalamila well known as "Ray C" has been admitted to Rehab........


Report from 'msn african'


Facebook waja na "VERIFIED ACCOUNT" Uhuru Kenyatta awa wakwanza. . . . . . . . .

Facebook imefuata mkondo Twitter kwa kuanzisha akaunti na kurasa zilizothibitishwa (verified pages/accounts) ili kuwawezesha watu mashughuli kuthibitisha akaunti akaunti na fan page zao. Facebook wamesema wamefanya hivyo ili kusaidia watumiaji wa Facebook kuzitambua akaunti za kweli za mastaa na watu wengine mashughuli wanaotumia mtandao huo, pia ikiwemo biashara zenye majina makubwa.

Kurasa zilizothibitishwa zitakua na alama ya blue ya pata “check-mark” kama inavyoonekana kwenye picha hapo juu. Watu wataoruhusiwa kutumia huduma hiyo ni, viongozi wa serikali, waandishi wa habari maarufu, makampuni au bidhaa maarufu. Hivyo kuanzia sasa, utaweza kufahamu akaunti/pages zipi ni za kweli na zipi ni feki.

Ili mtu mashughuli kupata akaunti iliyohakikishwa, mhusika atahitaji kuwasilisha kitambulisho halali kinachotambuliwa kiserikali. Nadhani celebrities (mastaa) Wengi wa Afrika wataipenda hii. Kama mfano Wema, kuna page zaidi ya kumi zinazodai kuwa ni “Wema Sepetu”



Katiba Mpya, kuzinduliwa rasmi tarehe 3 juni saa nane mchana........

Tume ya Mabadiliko ya Katiba inapenda kuwafahamisha wananchi wote kuwa itafanya uzinduzi wa Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania siku ya Jumatatu, Juni 3, 2013, kuanzia saa 8:00 mchana katika viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam.
Uzinduzi huo utarushwa moja kwa moja na vituo vya redio vya TBC Taifa, ZBC Redio na vituo vya televisheni vya TBC 1 na ZBC TV na vituo vinginevyo vya redio na televisheni.
Rasimu hiyo ya Katiba imetokana na maoni ya wananchi, viongozi na makundi mbalimbali waliyowasilisha kwa Tume kupitia njia mbalimbali zikiwemo mikutano, barua pepe, ujumbe mfupi wa simu za mikononi (sms) na nyinginezo.
Tume inawaomba wananchi na wadau kufuatilia uzinduzi huo kwa makini kupitia vyombo hivyo vya habari.
Mwisho.
 
Imetolewa na:
Noel Kapinga Jr.

Wasanii walipokutana Leaders (May 29) kuchangisha fedha za msiba wa Albe...



Ndani ya viwanja vya leaders, wasanii wa bongo flava akiwemo Prof. jay pamoja na dume la simba Afande sele wakati wa kuchangisha fedha kwaajili ya msiba wa Albert Mangwea maarufu kama "Ngwair"